Arusha
Home » » MKUTANO MKUBWA WA KIMATAIFA WA TAASISI YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI TANZANIA (CILT) KUFANYIKA MACHI, 3 JIJINI ARUSHA‏

MKUTANO MKUBWA WA KIMATAIFA WA TAASISI YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI TANZANIA (CILT) KUFANYIKA MACHI, 3 JIJINI ARUSHA‏


 Balozi wa Heshima wa Taasisi ya Kimataifa ya Usafirishaji na Uchukuzi Tanzania (CILT), Waziri wa Jumuia ya Afrika Mashariki, Dk. Harrison Mwakyembe (kulia), akizungumza katika mkutano wa maandalizi ya kukusanya fedha kwa ajili ya mkutano wa kimataifa utakaofanyika jijini Arusha kuanzia Machi 4 hadi 5 ulioandaliwa na taasisi hiyo kwa ajili ya kuwajengea weredi wadau wa usafirishaji kutoka nchi mbalimbali duniani. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi kutoka Cilt, Zacharia Hans Poppe.
 Mwenyekiti wa CILT, George Makuke (kushoto), akizungumza katika mkutano huo. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Mipango wa MOT, Migire Gabriel, Balozi wa Heshima wa Taasisi ya Kimataifa ya Usafirishaji na Uchukuzi Tanzania (CILT), Waziri wa Jumuia ya Afrika Mashariki, Dk. Harrison Mwakyembe na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi kutoka Cilt, Zacharia Hans Poppe.
Mkurugenzi wa Mipango wa MOT, Migire Gabriel, akizungumza katika mkutano huo.
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye mkutano huo.
Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.

Dotto Mwaibale

IMEELEZWA kuwa ukosefu wa weledi na utaalam wa masuala mbalimbali ya usafirishaji ndio chanzo cha kutokea kwa ajili nyingi nchini.

Hayo aliyasema jana Dar es Salaam Mwenyekiti wa Taasisi ya Kimataifa Usafirishaji na Uchukuzi nchini(FCILT), George Makuke wataki wakizungumzia maandalizi ya mkutano mkubwa unaotarajiwa kufanyika Machi mwaka huu Mkoani Arusha.

Mkutano huo utahusisha nchi mbalimbali Duniani ukiwa na lengo la kujenga weledi katika masuala ya usafirishaji na uchukuzi.

Akizungumzia mkutano huo alisema kuna mambo mengi yanafanyika katika usafirishai ambayo si sahihi hivyo mkutano huo utasaidia wahusika kutoa huduma kihalali.

"Ukiangalia kumekuwa na udanganyifu mkubwa katika masuala ya usafirishai kwa kuzidisha bei lakini hata watoa huduma wenyewe wamekuwa hawana weledi hivyo mkutano huo utajadili namna ya kuondia changamoto zote hizi"alisema 

Kwa Upande wa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Harrison Mwakyembe alisema kuwa mkutano huo ni mkubwa hivyo atahamasisha taasisi mbalimbali kutoa michango yao kwani unahitaji fedha nyingi kwaajili ya kuwahudumia wageni.

"Hasa nitaangalia namna gani taasisi za Wizara ya Maliasili na Utalii wamechangia kiasi gani maana wao ndio watakaofaidika kwani watu watatoka nchi mbalimbali hivyo itasaidia kuitangaza nchi"alisema 

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano huo,Zakaria Hans pope, alisema mkutano huo utasaidia kukuza uchumi kwani kama kukiwepo njia sahihi za usafirishaji mapato lazima yaongezeke. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)<
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa