Arusha
Home » » NAIBU MKURUGENZI MKUU WA UNESCO AWASILI JIJINI ARUSHA KUSHIRIKI MAHAFALI TAASISI YA MANDELA

NAIBU MKURUGENZI MKUU WA UNESCO AWASILI JIJINI ARUSHA KUSHIRIKI MAHAFALI TAASISI YA MANDELA


DSC_0499
Ofisa mwandamizi wa habari na mahusiano ya umma wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Bw. Karimu Meshack (kushoto) akijadiliana jambo ndani chumba cha mapumziko cha wageni mashuhuri na Mwakilishi mkazi shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues pamoja na Afisa mipango kitaifa, kitengo cha Sayansi UNESCO,Tanzania, Gabriela Lucas kabla ya kuwasili kwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Getachew Engida.
DSC_0516
Mwakilishi mkazi shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues akimlaki Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Getachew Engida wakati alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ajili kuhudhuria mahafali ya pili ya Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela jijini Arusha yanayofanyika kesho. Kulia ni Ofisa mwandamizi wa habari na mahusiano ya umma wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Bw. Karimu Meshack na wa pili Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, Dr. Moshi Kimizi.
DSC_0517
Mwakilishi mkazi shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues (katikati) akimlaki kwa furaha Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Getachew Engida (kushoto) aliyewasili jioni hii jijini Arusha na shirika la ndege la Ethiopia. Kulia ni Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, Dr. Moshi Kimizi.
DSC_0518
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Getachew Engida akisalimiana na Ofisa mwandamizi wa habari na mahusiano ya umma wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Bw. Karimu Meshack kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
DSC_0524
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Getachew Engida akiwa na mwenyeji wake Mwakilishi mkazi shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues mara baada ya kuwasili wakielekea kwenye chumba cha mapumziko cha wageni mashuhuri.
DSC_0526
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa