Arusha
Home » » WATUHUMIWA WA MABOMU ARUSHA MAHAKAMANI TENA

WATUHUMIWA WA MABOMU ARUSHA MAHAKAMANI TENA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Watuhumiwa 19 wanaotuhumiwa kulipua bomu kwenye viwanja vya Soweto, wamepandishwa kizimbani kwa mara ya pili mbele ya hakimu Hawa Mguruta na hawakutakiwa kujibu chochote.
Washitakiwa hao waliomba mahakama iwaruhusu kuonana na ndugu zao, ili wawape maagizo ya kifamilia.

Aidha, walidai mtuhumiwa mmoja ni mgonjwa na daktari alimpa maagizo ya kula aina maalum ya chakula, ila tangu apelekwe gerezani hapati chakula zaidi ya mchicha mchemsho na maharage, hali inayosababisha wakati mwingine kupoteza fahamu.

Hakimu Mguruta akijibu hoja hizo, alisema suala la ndugu zao kwenda mahakamani kuwaangalia lipo juu ya uwezo ila wanaweza kufuata taratibu za magereza kwa kuandika barua na kuomba kama itawezekana.

Kesi hiyo iliahirishwa hadi Agosti 29 mwaka huu, itakapotajwa tena.

Awali  Mawakili wa serikali waliwasomea mashitaka yao kwa kupokezana ambao ni Augustino Kombe, Marcelino Mwamunyange na Felix Kwetukia, walidai mahakamani hapo, washitakiwa hao wanashitakiwa kwa kula njama ya kufanya ugaidi, kufadhili kufanyika kwa ugaidi.

Makosa mengine ni kufanya mauaji baada ya kutupa bomu, kusababisha majeraha, kutoa ushirikiano kufanyika kwa ugaidi, kukusanya dhana ili kutenda ugaidi na kusambaza dhana ili kutenda ugaidi.

Walidai kuwa washitakiwa hao wanadaiwa kufanya makosa hayo Julai 3 mwaka huu, Juni 15, kwenye viwanja vya Soweto, katika mkutano wa Chadema na kusababisha mauaji na majeraha kwa watu. Pia walidai kuwa washitakiwa hao Juni 23, 24 na Julai 21 mwaka huu, walikusanya mabomu saba ya kurusha kwa mkono kwa lengo la kuwezesha kufanyika kwa ugaidi.

SOURCE: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa