Arusha
Home » » WANACHAMA VICOBA WASHAURIWA

WANACHAMA VICOBA WASHAURIWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Arusha Namelok SokoineWANACHAMA wa vikundi vya kuweka na kukopa (VIKOBA) mkoani Arusha wametakiwa kupanga na kutumia vizuri fedha wanazokusanya ili ziwasaidie kutoka daraja moja hadi jingine katika maisha yao.
Kauli hiyo ilitolewa mkoani hapa na Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Arusha Namelok Sokoine alipoendesha harambee ya utunishaji wa fedha kwa umoja wa wanavikoba wa Engutoto yenye vikundi 20 na wanachama 600.
Katika utunishaji huo, Namelok alichangia sh milioni 10 huku sh milioni 12 ikipatikana katika shughuli hiyo iliyohudhuriwa na viongozi wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) wilayani Monduli.
“Wanawake nawaomba muendelee kujitokeza na kujiunga katika vikoba kwani huku ndipo tutaweza kuwa na sauti ya kujitegemea kimapato.
“Lakini pia naomba niwakumbushe jambo muhimu hizi fedha tunazokusanya nawaomba muonyeshe mfano wa kuzitumia vizuri ili kesho zitusaidie kutoka daraja moja kwenda jingine kiuchumi,” alisema Namelok.
Naye Katibu wa UWT Engutoto Glory Emmanuel alisema “Tunaomba suala la ofisi za vikoba uliangalie kwani vikundi havina ofisini. Wanachama wengi hawana elimu hali inayosababisha kukopa na kutumia fedha vibaya,” alisema Glory.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa