Arusha
Home » » HIVI NDIVYO MWANAMUZIKI NYOTA WA NYIMBO ZA DINI ALIVYO PONA KATIKA AJALI HII.

HIVI NDIVYO MWANAMUZIKI NYOTA WA NYIMBO ZA DINI ALIVYO PONA KATIKA AJALI HII.


Gari likiwa limepinduka bondeni.
Mwimbaji anayetamba na wimbo wa "Zawadi gani nitamtolea BWANA" ambaye pia ni mtume akichunga kanisa jijini Dar es Salaam John Komanya amepata ajali mbaya juzi mchana maeneo karibu na daraja la Mto Wami akiwa njiani kuelekea mkoani Arusha kukutana na viongozi wanaohudumu na mwalimu Christopher Mwakasege, kwa ajili ya mkutano wa injili ambao utakuwa na lengo la kuombea taifa kwa siku nne mwezi Disemba.
Akizungumza na GK mtume Komanya amesema lengo lilikuwa ni kupeleka barua kwa viongozi hao ili wamfikishie mwalimu Mwakasege kwaajili ya mkutano huo. Amesema akiwa njiani katikati ya Msata na Wami na wakati huo hakuwa amefunga mkanda wa gari, ndipo akasikia sauti ya Roho Mtakatifu ikimwambia kwa upole afunge mkanda lakini akawa anapuuzia na kuanza kujiuliza kwanini, sauti ikarudia tena kwa upole ikimwambia afunge mkanda akiwa bado anajiuliza ndipo anasema akasikia sauti ya Mungu ikizungumza kwa haraka na ukali "John funga mkanda" ndipo akafunga mkanda.

Mtume Komanya amesema akiwa anateremka kuelekea wami akiwa katika mwendo wa 180 wakati akipita katika kona kulikuwa na malori matatu mbele yake kukawa na lori lingine likifuatiwa na mabasi matatu yakipandisha kutoka Arusha kuja Dar, kwa wakati huo aliona malaika saba ambapo walishuka mithili ya makomandoo washukavyo kutoka kwenye kamba ya helikopta, mmoja akiwa amekaa kwenye boneti mbele, mwingine kulia, kushoto na mwingine nyuma yake ambaye alimwambia Komanya afuate maelekezo yake, anasema akiwa anamwangalia malaika aliyekaa karibu naye katika kiti cha dereva aliambiwa afuate maelekezo anayopewa na malaika wa nyuma yake.

Alipokuwa akiangalia mbele akaona gari linayapita mengine kwa spidi hali iliyomfanya Komanya kutaka kuingia katikati ya magari mengine lakini malaika akamwambia afuate maelekezo yake na kuambiwa aachie uskani jambo ambalo alilipinga kwakuwa aliona kifo mbele yake na kutaka kuingia katikati ili kukwepa, lakini malaika akamwambia ukiingia katikati utakufa, wewe achia usukani kama ninavyokwambia kwakuwa wametumwa kumlinda, akawa bado anatafakari kutokana na kuliona korongo kubwa upande wake huku malaika wakimwambia asiguse kitu chochote ikiwemo kutokanyaga breki lakini bila kusikia akakanyaga na kusababisha gari kuyumba sana, malaika akamwambia tena aachie breki na kuweka mikono yake kifuani. Anasema alipoweka mikono kifuani aliona wakiligonga lori huku malaika akiwa ameshika usukani na kuonyonga sana huku yeye akisema alijikuta akiwekwa kwenye kitu kama chupa ya maji, na yeye kwa wakati huo kuona kama vile yupo ndani ya glasi ya maji, ila anaona kinachoendelea.
Kisha baada ya hapo, upande wake wa usukani ndio uliogongwa, mara baada ya malaika kuchezesha usukani kidogo ili kuepusha madhara zaidi, na kisha ile semi-trailler ikamtupia kwenye korongo na kubinuka mara tatu hewani kabla ya kutua chini kwa mara ya nne, ambapo gari ilikuwa juu chini, yaani matairi yakiwa yanatazama juu.
Baada ya hapo kilichofuata ni kuendelea kusikiliza malaika wasemacho, ambapo hapo alisikia sauti ikisema fungua mkanada utoke, na kwa wakati huo kulikuwa na moshi ullioanza kutoka kwenye gari - na hapo akapewa dakika 12 kuchukua baadhi ya vitu alivyokuwa navyo kwenye gari. Maajabu ya Mungu, hakuna kitu chochote kilichogusa mwili wake, na wala hakuna damu iliyovuja kutokana na gari hilo kupindukia kwenye korongo.
Hakika utukufu ulimrudia Mungu kwa wakati huo kwani baadhi ya mashuhuda walikiri hapohapo ya kwamba hakuna mtu anayeweza kusalimika kwenye ajali hiyo, bali ni lazima tu mkono wa Mungu umehusika hapo kuokoa.
Baadhi ya mashuhuda ambao walikuwapo kwenye mabasi ya mkoa (hadi mkoa) walimtambua mtumishi wa Mungu ya kwamba ni John Komanya na hatumaye kumshukuru Mungu hapohapo, ambapo baadae Polisi walifika kwa ajili ya kazi yao - lakini hilo halikumzuia Mchungaji Komanya kupiga magoti na kumshukuru Mungu licha ya umati wa watu - na tukio hilo liliambatana na yeye kuisikia sauti ya Mungu ikimwambia "Nimekupa kazi ya kutengeneza kanisa langu,... usiogope nitakulinda, ila kuwa mwaminifu na nitakuweka kwenye uaminifu"
Sauti hiyo ilitoka kwa kiumbe ambacho kilikuwa na muonekano wa malaika, Pastor Komanya anaieleza GK na kusema kuwa sauti yake ilikuwa ya tofauti, na mavazi yake yalikuwa ni meupe na kwamba alielezwa dhahiri kuwa hiyo semi trailer ilikuwa imetumwa kummaliza, lakini ndio maana malaika walitumwa kumlinda.
"Zawadi Gani" kama ambavyo alikuwa akiitwa akiwa hospitali ya Muhimbili, alifanyiwa vipimo na kuonekana ya kwamba hana shida yoyote. Na hili linadhihirika hata pale alipotoka kwenye gari lililopiinduka, kwa kuwa alitoa vifaa vyake na kuanza pia kupiga picha, picha ambazo kama mtu akiziona zote, hakika hawezi kuamini kama kuna kusalimika hapo.
Mwisho wa yote Mchungaji Komanya anakiri kuwa amepona kwa rehema ya Mungu, na baada ya hapo amemuahidi kumtumikia kwa kazi aliyompa licha ya kwamba ni ngumu na ina vikwazo vingi. Jumapili hii, Mchungaji Komanya ataimba wimbo mpya kumshukuru Mungu kutokana na kumuepusha na kifo. Kwa wasafiri wote, hapa kuna funzo la kujikabidhi mikononi mwa BWANA kila mara safari inapotokea, katu tusienende kwa mazoea.PICHA ZOTE NA GOSPEL KITAA BLOG


1 comments:

Unknown said...

Kama si BWANA Aliyekuwa Pmaoja nawe KOMANYA Na Useme sasa.....
MWACHENI MUNGU AITWE MUNGU, KWAKUWA YEYE NI MUNGU wa miungu YOTE.
MUNGU NI MUNGU WA KUOGOFYA..
KUMTEGEMEA NA KUMTUMIKIA MUNGU NI FAIDA KUBWA.
JAMAAAN WATU WA MUNGU TUWE WATII KWA SAUTI YA ROHO MTAKATIFU.

Ibrahim Mwakapola
0768 504232
Arusha-Tanzania

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Arusha Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa