ARUSHA.
MKUTANO wa Chadema wa kumaliza kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani mjini Arusha, jana ulivunjika baada ya bomu kulipuka na kuua watu wanne na wengine kujeruhiwa.
MKUTANO wa Chadema wa kumaliza kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani mjini Arusha, jana ulivunjika baada ya bomu kulipuka na kuua watu wanne na wengine kujeruhiwa.
Bomu hilo lililipuka jana saa 11:50 dakika chache
kabla ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Freeman Mbowe kumaliza
kuhutubia mkutano huo uliofanyika katika Viwanja vya Soweto mjini Arusha
na kuhudhur
iwa na mamia ya wananchi.
Hilo ni tukio la pili la bomu kulipuka katika
mkusanyiko wa watu, Mei 5 mwaka huu bomu lililipuka katika Kanisa
Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasit mjini Arusha
na kuua watu watatu na wengine kujeruhiwa.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru Frida Mokiti alisema katika hospitali yake kuna maiti moja ya mtoto na majeruhi 11.
Habari zingine zilisema katika hospitali ya
Misheni ya Selian kuna maiti za watu wawili, waliokufa kutokana na
shambulio hilo na majeruhi ambao idadi yao haijafahamika.
Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Arusha, Liberatus Sabas alisema katika tukio hilo watu wawili wamepoteza
maisha, mwanamke na mwanamume na kwamba idadi ya majeruhi bado
haijafahamika kwa kuwa wametawanywa katika hospitali mbalimbali mkoani
humo.
Watu walioshuhudia tukio hilo waliliambia gazeti
hili kuwa bomu hilo lililipuka karibu na jukwaa walilokuwa wamekaa
viongozi wa Chadema, wakati Mbowe na Mbunge wa Arusha mjini Godbless
Lema wakiwa katika hatua za kumaliza kuhutubia.
Taarifa zilidai kuwa kuna mtu alionekana akirusha
kitu kinachodaiwa bomu kwenye eneo la jukwaa karibu na gari la matangazo
la chama hicho, lakini alipokuwa akifuatiliwa baada ya kutokea mlipuko
huo, polisi nao walikuwa wameanza kudhibiti watu kwa kulipua mabomu ya
kutoa machozi na kupiga risasi za moto hali iliyozidisha taharuki.
Baada ya tukio hilo watu waliokuwa katika mkutano
huo walitawanyika wakikimbia kuokoa maisha yao huku wakimwacha Mbowe na
Lema na viongozi wengine wakiwa bado wako jukwaani.
Hali hiyo ilifanya barabara zote za mji wa Arusha kujaa watu waliokuwa wakikimbia ovyo.
Hali hiyo ya watu kukimbia ovyo kuliwafanya askari
polisi wengi kuingia mitaani kudhibiti watu na hivyo nao kulazimika
kutumia mabomu ya machozi hali ambayo ilizidisha taharuki.
Baadhi ya watu waliojeruhiwa walikimbizwa katika
Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru na wengine katika Hospitali ya Seliani
na wafuasi wa Chadema na watu wengine waliokuwa katika eneo hilo.
CHANZO MWANANCHI.
0 comments:
Post a Comment